Pata taarifa kuu

Ufaransa kuwaondoa raia wake nchini Niger

Nairobi – Ufaransa inatarajiwa kuaanza kuwaondoa raia wake kutoka Niger, ambapo mapinduzi ya wiki iliyopita yamesababisha maandamano ya kupinga Ufaransa, ubalozi wa Paris mjini Niamey umeeleza.

Ufaransa imesema itaanza kuwaondoa raia nchini Niger kutokana na mapinduzi ya kijeshi
Ufaransa imesema itaanza kuwaondoa raia nchini Niger kutokana na mapinduzi ya kijeshi REUTERS - STRINGER
Matangazo ya kibiashara

Niger imekuwa nchi ya tatu katika ukanda wa Sahel katika kipindi cha chini ya miaka mitatu kushuhudia mapinduzi baada ya Mali na Burkina Faso.

Utawala wa Rais Mohamed Bazoum uliangsuhwa  wiki iliyopita na wanajeshi maalum kutoka katika kikosi chake cha walinzi.

Mahamat Idriss Déby wa Chad ametajwa kuwa miongoni mwa watu wanaojaribu kuleta upatanishi nchini Niger
Mahamat Idriss Déby wa Chad ametajwa kuwa miongoni mwa watu wanaojaribu kuleta upatanishi nchini Niger © Présidence tchadienne

Watu wenye silaha wamekuwa wakitekeleza mashambulio dhidi ya raia wa mataifa hayo hali ambayo imechangia kuyumba kwa uchumi wake, baadhi ya mataifa ya ukanda huo yakitajwa kuwa mojawapo ya nchi maskini zaidi duniani.

Waandamanaji walionekana wakiwasha moto nje ya lango la ubalozi wa Ufaransa nchini Niger hali hii ikitajwa kuwa mojawapo ya Ufaransa kutangaza kuwaondoa raia wake.

Viongozi wa Afrika Magharibi, wakiungwa mkono na washirika wao wa Magharibi, walitishia kutumia nguvu kurejesha utawala wa rais Bazoum uliyochaguliwa kwa njia ya kidemokrasia na kutangaza vikwazo vya kifedha kwa wanajeshi waliohusika na mapinduzi hayo.

Uongozi wa ECOWAS umetaka kurejeshwa kwa utawala wa kiraia  nchini Niger
Uongozi wa ECOWAS umetaka kurejeshwa kwa utawala wa kiraia nchini Niger © AFP/Kola Sulaimon
Utawala wa kijeshi nchini Mali na  Burkina Faso ilionya kuchukua hatua iwapo njia za kijeshi zitatumika kurejesha utawala ulionagushwa nchini Niger.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.