Pata taarifa kuu
Kenya-Ufaransa

Shirika la maendeleo la Ufaransa AFD lashirikiana na serikali ya Kenya kubadilisha maisha ya raia

Nairobi – Shirika la maendeleo la Ufaransa AFD kwa ushirikiano na serikali ya Kenya imefanya miradi kadhaa iliyogharimu takribani Euro milioni 135 ili kuimarisha maisha ya wakenya wanaoishi kwenye mitaa ya mabanda jijini Nairobi na hata katika  miji mingine kama Kisumu .

Eneo la taka katika mtaa wa Kayole Soweto
Eneo la taka katika mtaa wa Kayole Soweto © Florence Kiwuwa
Matangazo ya kibiashara

Shirika hilo la ufaransa limewekeza mamilioni ya fedha ili kujenga barabara,kuweka mifereji ya maji , kuunda mitaro ya kupitisha maji chafu na kuweka taa za barabarani katika juhudi za kuimarisha maisha ya wakenya katika maeneo tofauti tofauti kama vile Kayole Soweto.

RFI imefanikiwa kuzungumza na Mkurugenzi wa shirika hilo kwenye ukanda wa Afrika, Helene Ngernim-Ganga  ili kueleza zaidi kuhusu shirika lao AFD na nini malenge yao 

Kwa sasa tunafanya kazi  na tuna miradi mingi ya maendeleo ,miundombinu ,nishati ,miradi ya  utoaji maji safi na usafi wa mazingiria kwa jumla.Pia tumewekeza kwa kiasi cha Zaidi ya asilimia 50  na tunazidi kukua katika sekta za kijamii kama vile elimu na afya.Alisema Helene Ngernim-Ganga

 

00:28

HELENE GANGA DIRECTOR AFD

 

Katika mtaa huo wa Kayole Soweto nilizungumza na Jane Wangare ambaye amefaidika pakubwa na mradi huo wa barabara na taa

00:25

JANA WANGARE MKAAZI SOWETO

Vilevile Hezron Ongesa anayesimamia  kundi la vijana katika eneo hilo amelisifu shirika hilo kwa kutoa ajira kwa zaidi ya vijana 200

00:16

HEZRON ONGESA MKAAZI SOWETO

 

Kufikia sasa AFD imewekeza euro milioni 35 huku benki kuu ya dunia ikitoa euro milioni 100 ili kufanikisha miradi hiyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.