Pata taarifa kuu

Marekani imetangaza vikwazo dhidi ya majenerali wawili wanaopigana nchini Sudan

NAIROBI – Marekani, imeziwekea vikwazo kampuni zinazohusishwa majenerali wawili wanaopigana nchini Sudan, katika mkakati wa kumaliza vita hivyo jijini Khartoum na nje.

Jeshi la serikali ya Sudan na wapiganaji wa RSF wamekuwa wakikabiliana kwa muda sasa licha ya wito wa kusitisha mapigano
Jeshi la serikali ya Sudan na wapiganaji wa RSF wamekuwa wakikabiliana kwa muda sasa licha ya wito wa kusitisha mapigano © Forces armées soudanaises / via Reuters
Matangazo ya kibiashara

Wizara ya fedha Marekani ,imesema imelenga kampuni kubwa mbili zinazohusishwa na jeshi na pia wapiganaji wa kikosi cha RSF na ambazo zinatuhumiwa kuchangia mapigano hayo nchini Sudan.

Kampuni hizo ni pamoja na  Al Junaid Multi Activities Co Ltd  na Tradive General Trading,  zinazohushwa na RSF na  Defense Industries System  na  Sudan Master Technology, zinazohushwa na jeshi la Sudan.

Waziri wa fedha wa Marekani ,Janet Yellen amesema lengo kubwa ni kukata ufadhili unaochochea vita hivyo.

Hatua hii inajiri baada ya pande zote kushindwa kuheshimu makubaliano ya kusitisha vita na kuruhusu usambazaji wa msaada.

Alhamis ya wiki hii ,watu 18 waliwauwa na wengine 100 kujeruhiwa ,katika shambulio la roketi kwenye soko moja jijini Khartoum.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.