Pata taarifa kuu

Umoja wa mataifa umeongeza muda wa vikwazo kwa Sudan Kusini

NAIROBI – Baraza la usalama katika umoja wa mataifa limeongeza muda wa vikwazo vilivyoekewa Sudan Kusini kuhusu silaha kwa kipindi cha mwaka mmoja zaidi, baadhi ya watu binafasi nchini humo pia wakiwa wameekwa vikwazo vya usafiri na mali zao kuzuiwa.

Salva Kiir, Rais wa Sudan Kusini
Salva Kiir, Rais wa Sudan Kusini AP - Brian Inganga
Matangazo ya kibiashara

Baraza hilo lilipiga kura siku ya Jumanne ya wiki hii, kura kumi zikipigwa kuidhinisha hatua hiyo, wanachama wengine watano wakikosa kupiga kura.

Katika uamuzi wake, baraza hilo limezitaka nchi wanachama wa umoja wa mataifa kuzuia uuzaji wa  moja kwa moja wa silaha au usafirishaji wa silaha kupitia nchi nyengine kwa taifa hilo la Sudan Kusini.

Vikwazo vya silaha viliongezwa hadi Mei mwaka ujao, huku baraza hilo likielezea wasiwasi wake juu ya kuendelea kuongezeka kwa ghasia na mzozo wa kisiasa wa muda mrefu.

Hali mbaya ya kiusalama, kiuchumi na  na hali ya kibinadamu katika maeneo mengi ya nchi hiyo pia ikielezwa kuwa mbaya. Nchi zilizosusia ni China, Russia, Ghana, Gabon na Msumbiji.

Balozi Akuei Bona Malwal kutoka Sudan Kusini amekashifu hatua hiyo  akisema "ilifanyika kwa nia mbaya ikiwa na malengo mabaya

Licha ya makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwaka 2018, ghasia zinaendelea na hadi kufikia Aprili mwaka huu watu milioni 2.3 nchini Sudan Kusini wamethibitishwa kuwa wakimbizi wa ndani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.