Pata taarifa kuu

Sudan: Tutatekeleza mkataba wa usitishaji mapigano: Kiongozi wa RSF

NAIROBI – Kiongozi wa kundi la wapiganaji wenye nguvu nchini Sudan la RSF, Mohamed Dagalo, akisema wapiganaji wake watatekeleza mkataba wa usitishaji mapigano ulioanza kufanya kazi hapo jana baada ya kutiwa saini mwishoni mwa juma mjini Jeddah, Saudi Arabia.

Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo, Kiongozi wa RSF nchini Sudan
Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo, Kiongozi wa RSF nchini Sudan REUTERS - MOHAMED NURELDIN ABDALLAH
Matangazo ya kibiashara

Baada ya kuzuka hofu kuhusu mahali aliko tangu kuanza kwa vita hiyo mwezi uliopita, Dagalo kupitia rekodi ya sauti, amezipongeza jumuiya za kikanda na hasa Saudi Arabia, kwa kusimama imara kutafuta suluhu ya mzozo unaoendelea kati yake na Jenerali, Abdel Fattah al Burhani.

Kauli yake imekuja siku chache kupita tangu afutwe kazi na Burhani kama naibu wake, ambapo pia akaunti za benki za kundi lake zimezuiliwa, kitendo ambacho mwenyewe amekikashifu.

"Tutaendelea kuwajibika kwa usalama wa nchi yetu na sisi tunaamini vita hivi vililazimishwa kwetu pia tutawaajibisha watu waliohusika na mapinduzi pamoja na washirika wao ambapo walipindua na kupindisha njia ya demokrasia ambayo Sudan ilikuwa inaelekea." alisema Mohamed Dagalo.

00:36

Mohamed Dagalo, Kiongozi wa RSF nchini Sudan

Licha ya kuaanza  kutekelezwa kwa mkataba wa usitishaji wa vita nchini Sudan hapo Jumatatu ya wiki hii,  kumeendelea kuripotiwa makabiliano kwenye mji wa Khartoum, kati ya vikosi hasimu.

Kwa mujibu wa raia walioko kwenye mji huo, milio ya risasi na roketi imesikika usiku kucha, huku baadhi hata wakichapisha picha za video kupitia kwenye mitandao ya kijamii, zikionesha moshi ukiwa umetanda kwenye maeneo mengi.

Hali kala hii pia imeripotiwa kwenye miji ya Omdurman na Bahri, ambapo nako mashuhuda wameripoti uwepo wa makabiliano.

Watu wenye silaha wanatembea mjini Khartoum mnamo Mei 22, 2023, huku mapigano kati ya majenerali wawili wapinzani yakiendelea. Milio ya risasi na milipuko iliutikisa mji mkuu wa Sudan Mei 22 asubuhi kabla ya usitishaji mapigano wa wiki moja kuruhusu missada ya  kibinadamu kuanza kuwafikia waathiriwa, ikiwa ni tukio la hivi punde baada ya misururu ya mapatano ambayo yote yamekiukwa. (Picha na AFP)
Watu wenye silaha wanatembea mjini Khartoum mnamo Mei 22, 2023, huku mapigano kati ya majenerali wawili wapinzani yakiendelea. Milio ya risasi na milipuko iliutikisa mji mkuu wa Sudan Mei 22 asubuhi kabla ya usitishaji mapigano wa wiki moja kuruhusu missada ya kibinadamu kuanza kuwafikia waathiriwa, ikiwa ni tukio la hivi punde baada ya misururu ya mapatano ambayo yote yamekiukwa. (Picha na AFP) © AFP

Baada ya wiki tano za mapigano kati ya jeshi la Serikali na vikosi vya RSF, pande hizo mwishoni mwa juma lililopita zilitiliana saini mkataba wa usitishaji vita kwa siku 7 kuanzia jana, ili kuruhusu misaada ya kibinadamu kuwafikia mamia ya raia walionaswa kwenye mapigano.

Kumekuwa na wasiwasi ikiwa makubaliano haya yatadumu, hasa ikizingatiwa kuwa saa chache kabla ya utekelezwaji wake hapo jana, jeshi lilifanya mashambulio ya anga kulenga ngome za RSF, huku kundi hilo likijibu hata baada ya muda wa makataa hayo kuanza.

Wanajeshi wa jeshi la Sudan wakiwa wamesimama karibu na gari kwenye barabara iliyofungwa mjini Khartoum Mei 20, 2023.
Wanajeshi wa jeshi la Sudan wakiwa wamesimama karibu na gari kwenye barabara iliyofungwa mjini Khartoum Mei 20, 2023. AFP - -

Makubaliano haya yameamsha tena matumaini ya vita kukoma, vita ambayo hadi sasa imesababisha raia zaidi ya milioni 1 na laki 1 kukimbia nyumba zao, wakiwemo laki 2 na elfu 50 waliokimbilia nchi jirani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.