Pata taarifa kuu

Sudan: Wawakilishi wa pande hasimu za kijeshi wanakutana nchini Saudi Arabia

NAIROBI – Saudi Arabia itakuwa mwenyeji wa mazungumzo ya kwanza ya ana kwa ana leo Jumamosi kati ya makundi mawili ya kijeshi yanayopigana nchini Sudan wakati huu mapigano yakiendelea kuripotiwa nchini humo licha ya kuwepo kwa wito wa kusitishwa.

Mkutano unaoleta pamoja pande hasimu za kijeshi nchini Sudan unafanyika nchini Saudi Arabia
Mkutano unaoleta pamoja pande hasimu za kijeshi nchini Sudan unafanyika nchini Saudi Arabia AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii ya Saudi Arabia inakuja wakati huu pia makubaliano ya awali yalioafikiwa na pande hizo hasimu za kijeshi ya kusitisha mapigano yakionekana kutibuka kwa mara kadhaa.

Kwa mujibu wa taarifa ya pamoja kutoka kwa nchi za Marekani na Saudia Arabia imeeleza kuwa kukaribisha kile imetaja kuwa majadiliano ya kabla ya mazungumzo huko Jeddah kati ya jeshi la Sudan na vikosi maalum vya RSF.

Mkutano huu wa kujaribu kupata suluhu ya kinachoendelea nchini Sudan unakuja wakati mapigano yakiendelea kuripotiwa katika baadhi ya miji nchini humo ikiwemo jiji kuu la Khartoum.

Picha iliyopigwa Mei 4, 2023 huko Khartoum, mji mkuu wa Sudan. Milio ya risasi na milipuko ilitanda Khartoum kwa siku ya 20 mfululizo, na kuacha juhudi za hivi punde za kusitisha mapigano.
Picha iliyopigwa Mei 4, 2023 huko Khartoum, mji mkuu wa Sudan. Milio ya risasi na milipuko ilitanda Khartoum kwa siku ya 20 mfululizo, na kuacha juhudi za hivi punde za kusitisha mapigano. AFP - -

Kwa mujibu wa jeshi la Sudan, mazungumzo hayo yanalenga masula muhimu yanayoibuka haswa suala la kibinadamu. Idadi kubwa ya raia jijini Sudan wameendelea kukabiliwa na changamoto ya ukosefu wa chakula na maji kutokana na mapigano hayo.

Wengi wa raia wa Khartoum wameeleza kukabiliwa na changamoto hizo, wakisema kuwa hawawezi kutoka nje kwenda kutafuta bidhaa hizo muhimu kwa kuhofia kushambulia.

Tayari jeshi la Sudan limethibitisha kuwatuma wajumbe wake mjini Jeddah kushiriki katika mazungumzo hayo, japokuwa vikosi vya RSF kwa upande wake havijatoa taarifa yoyote kuhusu suala hili.

Mohamed Hamdan Dagalo, Mkuu wa vikosi vya RSF Sudan
Mohamed Hamdan Dagalo, Mkuu wa vikosi vya RSF Sudan REUTERS - MOHAMED NURELDIN ABDALLAH

Umoja wa Mataifa na mashirika ya misaada yamekuwa yamekuwa yakieeleza kuwa huenda raia nchini humo wakakabiliwa na mzozo wa kibindamu iwapo mapigano hayo yataendelea.

Watu zaidi ya mia nne wamethibitishwa kufariki katika mapigano hayo ya wiki tatu, wengine zaidi ya laki nne wakiripotiwa kuyakimbia makazi yao.

Mataifa jirani na Sudan kama vile Chad na Sudan kusini yameripoti kuwapokea mamia ya raia wa Sudan wanaokimbilia katika mataifa hayo kutafuta hifadhi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.