Papa Francis kuwasili DRC leo Jumanne
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis, anatarajiwa kuwasili jijini Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia baadae leo, kuanza ziara ya kihistoria katika nchi hiyo baadaye siku ya Ijumaa atakwenda nchini Sudan Kusini.Jijini Kinshasa, maandalizi ya kumkaribisha Papa Francis yamekamilika, kama anavyoleza mwandishi wetu, Freddy Tendilonge
Imechapishwa:
Cheza - 01:50
Maafisa nchini humo, wanaendelea na juhudi za kujenga upya, sehemu ya jukwaa liliporomoka katika uwanja wa michezo wa Martyrs ambako Papa Francis atakuwa na misa kubwa siku ya Alhamisi.
Polisi wamesema sehemu hiyo iliporomoka kwa sababu ya upepo mkali jijini Kinshasa.