MAREKANI-AFRIKA -USHIRIKIANO
Waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen anazuru Afrika Kusini
Waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen, ameisifia Afrika Kusini kwa kuchukua hatua za madhubiti kushirikiana na nchi yake kuhusu mageuzi muhimu kwenye sekta yake ya nishati.
Imechapishwa:
Cheza - 00:28
Matangazo ya kibiashara
“Mnavyofahamu Afrika Kusini ni taifa la kwanza kubadilisha mfumo wake wa nishati kwa kushirikiana na Marekani. ”amesema Janet Yellen.
Hii imekuja, baada ya kushuhudiwa kwa maandamano ya maelfu ya watu hapo jana Jumatano kulalamikia kukatikakati kwa umeme kila wakati.
Ziara yake nchini Afrika Kusini imekuja, baada ya ziara ya Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi, Sergei Lavrov.