AFRIKA KUSINI - UMEME
Maandamano Afrika Kusini kulalamikia ongezeko la kukatika kwa umeme
Nchini Afrika Kusini, wafuasi wa chama cha Democratic Alliance (DA), wameandamana jijini Johannesburg, kulalamikia ongezeko la kukatika kwa umeme mara kwa mara nchini humo.
Imechapishwa:
Cheza - 00:29
Matangazo ya kibiashara
Waandamanaji walikwenda katika makao makuu ya chama tawala ANC, wakiwa na mabango yaliyosomeka, imetosha.
John Steenhuisen ni kiongozi wa DA.
“Maandamano ya leo ni mwanzo wa kurejesha nguvu kwa raia wa Afrika Kusini ambao ndiyo wenye nguvu.”amesema John Steenhuisen.
Afrika kusini kwa muda sasa imekuwa inakabiliwa na changamoto za kukatika kwa umeme, raia wakieleza kushindwa kuendelea na biashara zao za kila siku.