Pata taarifa kuu
RWANDA- SIASA- HAKI ZA BINADAMU

Human Rights Watch yadai Rwanda inakiuka haki ya kujieleza

Shirika la Kimataifa la kutetea haki za Binadamu la Human Rights Watch, linaishtumu Rwanda kwa kukiuka haki ya kujieleza na inataka kurekebisha sheria yake. 

Paul Kagame, Rais wa Rwanda
Paul Kagame, Rais wa Rwanda AFP - SIMON MAINA
Matangazo ya kibiashara

Hii inakuja baada kufungwa jela kwa mpinzani wa serikali ya Kigali, Théophile Ntirutwa kutoka chama cha Dalfa-Umurinzi, aliyekamatwa mwaka 2010 kwa madai ya kusambaza tarifa za uongo, zilizolenga kuichafua nchi hiyo. 

Lewis Mudge, ni Mkurugenzi Mkuu wa Human Rights Watch barani Afrika. 

“Imekuwa ni vigumu kwa mtu yeyote kuikosea serikali ya Rwanda.”ameeleza Lewis Mudge.

Taarifa ya HRW inakuja wakati huu baadhi wanasiasa wa upinzani katika baadhi ya mataifa ya Afrika wakizituhumu serikali zilizo madarakani kwa kuwahanagisha.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.