Pata taarifa kuu
DRC- USALAMA

DR Congo : Watu 10 wameuawa katika shambulio la bomu kanisani

Watu 10 wameripotiwa kuuawa wakiwemo watoto na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa, baada ya kutekelezwa shambulio la bomu kwenye kanisa moja mjini Kasindi katika mpaka wa DRC na Uganda, kilometa 80 kaskazini mwa mji wa Beni.

Wanajeshi wa Serikali ya DRC, wakiwa kwenye misitu ya Beni mashariki mwa DRC kuwasaka wapiganaji wa waasi wa Uganda, ADF ambao wanatekeleza mauaji ya kiholela
Wanajeshi wa Serikali ya DRC, wakiwa kwenye misitu ya Beni mashariki mwa DRC kuwasaka wapiganaji wa waasi wa Uganda, ADF ambao wanatekeleza mauaji ya kiholela UN Photo/Sylvain Liechti
Matangazo ya kibiashara

Waasi wa ADF wenye uhusiani na mtandao wa Al Qaeda wakitajwa kuhusika.

Luteni Mopero Momitabonge, ni kamanda wa polisi kwenye mji wa Kasindi.

Watu wameumia wengi, wengine wako hosipitalini zaidi ya kumi na wawili. amesema Mopero Momitabonge

Shambulio hili limetekelezwa licha ya operesheni za pamoja za kijeshi zinazoendelea kwenye eneo hilo dhidi ya waasi hao kati ya jeshi la serikali FARDC na lile la Uganda, UPDF.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.