Pata taarifa kuu
DRC- RWANDA-USHIRIKIANO

DR Congo yaijibu Rwanda kutokana na kauli yake kuhusu wakimbizi

Licha ya serikali ya Kigali kuweka wazi msimamo wake kuhusu kuendelea kuwapokea wakimbizi kutoka kwa majirani zake, serikali ya Kinshasa na yenyewe imejibu na kusema kuwa imegundua ujanja wake wa kutaka kuishinikiza Jumuia ya kimataifa kulipa gharama za kila mkimbizi kutoka DRC aliyeko huko Rwanda, kama ambavyo serikali yake ilikubaliana na Uingereza kuhusu wakimbizi waliopelekwa nchini mwake.

 Félix Tshisekedi,Rais wa DRC
Félix Tshisekedi,Rais wa DRC © Arsène Mpiana / AFP
Matangazo ya kibiashara

Patrick Muyaya ni msemaji wa serikali ya Kinshasa.

“Hadi Novemba mwaka wa 2022 idadi tulioipata inaonyesha kwamba wakimbizi elfu 77 kutoka Congo wapo nchini Rwanda na wamekuwa wakishawishiwa na serikali ya Rwanda wengi wao kwa bahati mbaya wamekuwa wakitumika kisiasa.”Ameeleza Patrick Muyaya

Kwa muda sasa Kinshasa imeendelea kuituhumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi wa M23 wanaoyumbisha usalama Mashariki ya DRC madai ambayo Kigali imeendelea kukana.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.