Pata taarifa kuu

Raia wa Burundi waokolewa nchini Uganda wakisafirishwa kimagendo

Jeshi la polisi nchini Uganda, linasema limefanikiwa kuwaokoa raia 24 kutoka Burundi, wengi wao wakiwa wanawake, ambapo walikuwa wakisafirishwa kimagendo kwa kisingizio cha kutafutiwa kazi nchini humo.

Polisi wakipiga doria Kampala, Uganda.
Polisi wakipiga doria Kampala, Uganda. AFP - BADRU KATUMBA
Matangazo ya kibiashara

Polisi imesema raia hao walikamatwa baada ya basi walilokuwa wakitumia kusafiri kutoka kwenye mpaka wa Mtukula kukamatwa katika njia kuu ya Kampala, asubuhi ya hivi leo.

Claire Nabakka ni naibu msemaji wa jeshi la polisi nchini Uganda.

“Kupitia uchunguzi tuliofanya tumebaini raia hawa ishirini na wanne kutoka Burundi waliletwa Uganda kufanya kazi za kawaida.” amesemaClaire Nabakka

Kwa mujibu wa mashirika ya kutetea haki za binadamu, yanasema biashara ya binadamu kwenye nchi za ukanda imeanza tena kushamiri, ikihusisha maofisa wa juu serikali na kwenye vyombo vya usalama, ambapo raia wamekuwa wakisafirishwa kwenda kufanya kazi katika nchi za kiarabu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.