Uganda: Watoto ni miongoni mwa watu tisa waliofariki kwa mkaganyano
Watu tisa, wenye umri kati ya miaka 10 na 20, wamepoteza maisha jijini Kampala nchini Uganda, baada ya kutokea kwa mkaganyano wa watu, wakati wa kuukaribisha mwaka mpya, usiku wa kuamkia jana katika jumba la biashara la Freedom City mall.
Imechapishwa:
Cheza - 00:52
Polisi wamesema, watu watano walipoteza maisha papo hapo, huku wanne wakifarifki wakikimbizwa hospitalini kwa kukosa pumzi, katika mkasa ambao pia, ulisababisha majeruhi ya watu kadhaa.
Polisi wameanzisha uchunguzi katika tukio hilo la usiku wa kuamkia mwaka mpya.
‘‘Polisi wanachunguza kuwepo kwa uzembe na uwamuzi wa haraka kwenye kisa kilichotokea kwenye jumba la freedom mall na kusababisha vifo vya watu tisa wakiwemo watoto saba’’. Amesema Luke Owoyesigyire.
Idadi kubwa ya raia duniani hukusanyika katika maeneo ya umma kusherekea mwaka mpya.