Pata taarifa kuu
Libya - siasa

Libya : Beltress laitisha maandamano Zaidi

Maandamano zaidi yanazidi kushuhudiwa nchini Libya, raia wakilalamikia kupanda kwa bei ya vyakula, ukosefu wa nguvu za umeme na mzozo wa kisiasa nchini humo.

Wandamanaji nchini Libya.
Wandamanaji nchini Libya. AP - Yousef Murad
Matangazo ya kibiashara

Vijana wenye hasira wameonekana wakiwasha magurudumu ya magari na kufunga barabara zikiwemo barabara kuu jijini Tripoli, Polisi wakikosa kuingia kati kutuliza hali .

Maandamano hayo yanaongozwa na vuguvugu kwa jina Beltress, ambalo linasema linapanga maandamano zaidi, kushinikiza kufanyika kwa uchaguzi na kuvunjwa kwa mabunge yote mawili ambayo yanahasimiana.

Mwishoni mwa juma lililopita wandanaji hao walivamia bunge la mashariki eneo la Tobruk, na kuteketeza sehemu ya jengo la bunge hilo

Taifa la Libya limekuwa kwenye mzozo tangu mwaka 2011, wakati kiongozi wa taifa hilo Moamer Kadhafi, aliondolewa madarakani na kuuawa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.