Tanzania na Uganda zatiliana saini mikataba kadhaa ya ushirikiano.
Uganda na Tanzania, zimetiliana saini mikataba kadhaa ya ushirikiano, ikiwa ni pamoja na Tanzania sasa kuendelea kununua sukari na dawa za kupunguza makalu ya maambukizi ya virusi vya ukimwi ARV’s kutoka nchini Uganda.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Leo hii katika ikulu ya Entebbe, tumempokea Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mheshimiwa @SuluhuSamia . Uganda inawakaribisha Mheshimwa Suluhu , akiambatana na mawaziri pamoja viongozi wa juu wa serikali ya Tanzania. Uganda enjoys a fraternal relationship with Tanzania. pic.twitter.com/rwaifMhxPh
— Yoweri K Museveni (@KagutaMuseveni) May 10, 2022
Hii imekuja, kufuatia ziara ya siku mbili ya rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan hapa Uganda ambapo Imekubaliwa kuwa Uganda itaiuzia Tanzania tani Elfu 10 ya sukari, hatua ambayo imemfurahisha rais Museveni na kuisifia nchi hiyo jirani.
Tangu tuingie Serikalini, tumekuwa tukifanya kazi vizuri sana na Serikali za Tanzania na viongozi waliokuwepo. Hatuna tatizo na Tanzania kwa sababu hakuna mvutano kati ya Tanzania na Uganda. Kwa hiyo kazi yetu ni kuzingatia zaidi usalama, miundombinu na biashara
Yoweri Museveni kuhusu biashara na Tanzania Mei 11 2022
Kauli hii imeungwa mkono na rais Samia, ambaye nchi yake imeingia kwenye mkataba na Uganda yakujenga bomba la mafuta kutoka Hoima mpaka bandari ya Tanga, ambao viongozi wanasema mchakato unaendelea vema licha ya kupingwa na waharakati wa mazingira na wale wa haki za binadamu.
Nchi zetu mbili zimeamua kulipea swala la Biashara na Uwekezaji kipau mbele. Hatua mahususi zitachukuliwa ili kurahisisha biashara kati ya nchi zetu hasa uondoaji wa vikwazo visivyo vya ushuru. Nawaalika Waganda kuja Tanzania kwa ajili ya kuongeza biashara na uwekezaji.
Samia Suluhu Hassan akiwa ziarani nchini Uganda Mei 11 2022
Yasin Nasser ni mfanyabiashara kutoka kampuni ya mafuta, anataka vikwazo zaidia vya kufanya biashara viondolewe.
Nadhani wanashugulikia vizuri bomba la mafuta itakua inaongeza biashara lakini muhimu tunataka wa punguze garama za barabarani.
Yasin Nasser mfanyabiashara
Takwimu zinaonesha kuwa kwa kipindi cha miaka 25 iliyopita, mauzo ya Uganda kwenda Tanzania yameongezeka kutoka Dola Milioni 2 nukta 6 hadi Dola Milioni 95.1. Nayo Tanzania, iliuza bidhaa vyenye thamani ya Dola Milioni 734 mwaka 2020.