Pata taarifa kuu
SUDAN-USALAMA

Sudan: Watu kadhaa wafariki dunia wakati wa maandamano ya kuunga mkono demokrasia

Katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum, maandamano mapya ya kuunga mkono demokrasia yamefanyika Jumamosi hii, Novemba 13, wiki tatu baada ya mapinduzi ya kijeshi ya Jenerali Abdel Fattah al-Burhan.

Waandamanaji wanaounga mkono demokrasia katika mitaa ya Khartoum. Jumamosi tarehe 13 Novemba 2021.
Waandamanaji wanaounga mkono demokrasia katika mitaa ya Khartoum. Jumamosi tarehe 13 Novemba 2021. AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Hali ni ya wasiwasi katika maeneo kadhaa ya mji mkuu wa Sudan, Khartoum, huku watu watano miongoni mwa waandamanji wakiripotiwa kufariki dunia.

Waandamanaji wengine wameuawa mjini Khartoum siku ya Jumamosi, na kufikisha idadi ya watu watano kutoka kambi ya upinzani wa mapinduzi waliouawa kwa kupigwa risasi na kurushiwa mabomu ya machozi na vikosi vya usalama, chama cha madaktari wanaounga mkono demokrasia umesema.

Makumi kwa maelfu ya Wasudan wanaendelea kupiga kelele "Hapana kwa utawala wa kijeshi" katika mitaa ya Khartoum na miji mingi nchini Sudan wakati wa maandamano nchini Sudan dhidi ya mapinduzi yaliyoongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhane.

"Watu wengi wamejeruhiwa kwa kupigwa risasi katika maeneo tofauti ya Khartoum", chama cha madaktari wanaounga mkono demokrasia kimeongeza.

Inarifiwa kuwa takriban waandamanaji 20 wameuawa tangu Oktoba 25.

Kisa cha urushaji wa gesi ya kutoa machozi kimeripotiwa huko Omdurman, magharibi mwa Khartoum.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.