Pata taarifa kuu
REUNION

Covid-19: Kisiwa cha Reunion chawekwa chini ya masharti ya watu kutotoka nje

Kuanzia wikendi hii na kwa muda wa wiki mbili, Visiwa vya Reunion vitakuwa chini ya masharti ya watu kutotembea mchana na sheria ya kutotoka nje usiku imetangazwa kuanzia saa 12 jioni hadi saa 11 Alfajiri.

Maelfu ya raia nchini Ufaransa waliandamana siku ya Jumamosi kupinga vizuizi vya kudhibiti kusambaa ugonjwa wa Covid-19 na sera za kuwalazimisha kudungwa chanjo.
Maelfu ya raia nchini Ufaransa waliandamana siku ya Jumamosi kupinga vizuizi vya kudhibiti kusambaa ugonjwa wa Covid-19 na sera za kuwalazimisha kudungwa chanjo. REUTERS - BENOIT TESSIER
Matangazo ya kibiashara

Kulingana na mkuu wa mkoa, maeneo kadhaa ya mji huo yanakabiliwa na "ongezeko lisilo kuwa la kawaida ya maambukizi ya visa vya Corona".

Hii ni mara ya kwanza tangu kutangazwa kwa hatua za watu kutotembea katika msimu wa majira ya Joto 2020. Kutokana na kuongezeka kwa kesi za Covid-19, Visiwa vya Reunion vimewekwa chini ya masharti ya watu kutotembea mchana, "kumetangzwa sheria ya kutotoka nje usiku kuanzia saa 12 jioni hadi saa 11 Alfajiri", hatua ambazo zitaanza kutekelezwa wikendi hii "kwa kipindi cha wiki mbili ", mkuu wa mkoa wa Reunion, Jacques Billant ametangaza Alhamisi jioni Julai 29.

Jacques Billant ametangaza pia kwamba mikahawa, baa na kumbi za michezo vitafungwa katika kipindi chote hicho cha wiki mbili.

Guadeloupe na Martinique zakabiliwa na ongezeko la maambukizi

Hatua hizi pia zitatekelezwa katika maeneo ya Antilles ya Ufaransa kama "Gaudeloupe na Martinique" ambapo kunaripotiwa ongezeko la visa vya maambukizi. Katika maeneo haya 17% tu ya raia ndio wamepewa chanjo wakati nchini Ufaransa 50% ya raia wamechanjwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.