Filipe Nyusi : Tutawashinda wanajihadi Cabo Delgado
Rais wa Musumbiji Filepe Nyusi, amesema ana matumaini serikali yake itawadhibiti wanajihadi wanaotatiza usalama kwa kuwaua raia katika mkowa wa Cabo Delgado.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Rais Nyusi, akizungumza wakati wa sherehe za 46 za uhuru wa taifa hilo, amesema wanajeshi wa taifa hilo kwa ushirikiano na wale kutoka nje, karibuni watalimaliza shughuli zote za wanajihadi katika mkowa Cabo Delgado.
Operesheni kali ya kuwasaka na kuwatokomeza wanajihadi hao itaendeshwa hivi karibuni, na usaidizi wa kutosha kutoka kwa mataifa ya SADC, na mengine yanayojali usalama wetu,’alisema rais Nyusi
Juma lililopita viongozi wa mataifa ya SADC, walikubaliana kuwatuma wanajeshi nchini Musumbiji, kulisaidia taifa hilo kutokemeza wanajihadi.
Katika mkutano huo, rais Nyusi, alitoa wito kwa mashirika ya kiraia kuendelea kusaidia raia wa Cabo Delgado, ambao wamekimbia makwao kutokana na shughuli za wanajihadi hao.