Pata taarifa kuu
DRC-RWANDA

DRC na Rwanda zakubaliana kuhusu masuala ya usalama na uchumi

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda, zimekubaliana kushirikiana kwenye maeneo matatu yenye umuhimu kati ya nchi hizo jirani.

Rais wa DRC Felix Tshisekedi akiwa na mwenzake Paul Kagame walipokutana mjini Goma Juni 26 201
Rais wa DRC Felix Tshisekedi akiwa na mwenzake Paul Kagame walipokutana mjini Goma Juni 26 201 © UrugwiroVillage
Matangazo ya kibiashara

Haya yamejiri baada ya kikao kati ya rais Felix Tshisekedi, na mwenzake Paul Kagame waliokutana mjini Goma siku ya Jumamosi.

Mikataba hiyo inahusu nchi hizo mbili kushirikiana na  kulinda miradi ya uwekezaji, kukomeshwa kwa utozwaji kodi mara mbili kwa bidhaa zinazovuka kati ya  nchi hizo mbili na ushirikiano wa kampuni za Aurifère du Kivu, Maniema (SAKIMA SA) na DITHER LTD.

Mbali na makubaliano hayo ya kiuchumi, viongozi hao pia  wamekubaliana  kushirikiana kwenye masuala ya usalama Mashariki mwa DRC, ili kuwezesha mazingira mazuri ya kufanikisha shughuli za maendeleo.

Viongozi hao wawili waliokutana mjini Rubavu upande wa Rwanda siku ya Ijumaa, kuthathmini madhara yaliyojitokeza kutokana na mlipuko wa Volkano,  siku ya Jumamosi, walitembelea eneo la Kibati, katika mkoa wa Kivu Kaskazini pia kuthathmini madhara yaliyojitokeza baada ya mlipuko huo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.