Pata taarifa kuu

Algeria: Imefuta Leseni ya Uendeshaji wa kituo cha Ufaransa ya 24

Serikali ya Algeria imesitisha leseni ya Televisheni ya Ufaransa France 24, siku moja baada ya uchaguzi wa wabunge, ambao wananchi wa taifa hilo la Afrika Kaskazini, wanasubiri matokeo.

France 24 ilisema viongozi wa Algeria wameipa onyo la mwisho mnamo Machi 13, kuhusu kupeperusha maandamano ya Ijumaa' ya harakati ya muda mrefu ya maandamano ya kupinga serikali ya Hirak
France 24 ilisema viongozi wa Algeria wameipa onyo la mwisho mnamo Machi 13, kuhusu kupeperusha maandamano ya Ijumaa' ya harakati ya muda mrefu ya maandamano ya kupinga serikali ya Hirak ALEXANDER KLEIN AFP/File
Matangazo ya kibiashara

Wizara ya Habari nchini humo imesema kuwa, imechukua hatua hiyo kwa kile inachoeleza kuwa, kituo hicho kimeendelea kushambulia taasisi za nchi hiyo.

Tangu tarehe 13 mwezi Machi  France 24 ilipokea onyo kutoka kwa serikali ya Algeria baada ya kupeperusha mandamano dhidi ya serikali ya taifa hilo la Afrika Kaskazini.

Hatua hii ya serikali ya Algeria, haijajibiwa na uongozi wa France 24 lakini mwezi Machi, Mkurugenzi Mkuu wa kituo hicho Marc Saikali, alisema kuwa Televisheni hiyo ilikuwa inafanya kazi yake ya uanahabari kwa kuheshimu sheria za nchi hiyo.

Serikali ya Ufaransa ambayo pia imekuwa na uhusiano baridi na Algeria, haijazungumzia kitendo hicho cha serikali ya Algers,wakati huu  serikali nchini humo ikiendelea kushutumiwa kuwahangaisha wanahabari wa nje na ndani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.