Pata taarifa kuu
ITALIA-DRC-USALAMA

Italia yataka UN kuchunguza mauaji ya balozi wake DRC

Serikali ya Italia, imesema imeomba Umoja wa Mataifa kuchunguza kwa kina kuuawa kwa Balozi wake Luca Attanasio, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wiki hii.

Balozi wa Italia DRC Luca Attanasio aliyeuawa katika shambulio la kuvizia Mashariki mwa DRC.
Balozi wa Italia DRC Luca Attanasio aliyeuawa katika shambulio la kuvizia Mashariki mwa DRC. © ITALIAN FOREIGN MINISTRY / AFP
Matangazo ya kibiashara

Balozi Attanasio ambaye mwili wake umerejeshwa nyumbani, alishalbuliwa na watu wenye silaha wanaotuhumiwa kuwa wa FDLR karibu na mji wa Goma wakati alipokuwa katika msafara wa Shirika la mpango wa chakula duniani WFP.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia Luigi Di Maio, katika hotuba yake kwa jopo la wabunge, alitoa maelezo ya awali ya namna shambulio hilo lilivyofanywa  akisema washambuliaji sita wanadaiwa kuwa waliyaamuru magari katika msafara huo kusimama kwa kuweka vizuizi barabarani na kisha walifyatua risasi kadhaa hewani.

Katika shambulio hilo, dereva wa mwakilishi huyo ambaye pia ni raia wa wa Italia aliuawa.  Waziri wa mambo ya kigeni wa Italia, Luigi Di Maio, aliliambia bunge la nchi yake kuwa wamewasilisha rasmi ombi kwa shirika la mpango wa chakula duniani pamoja na umoja wa mataifa  kuanzisha upelelezi utakaobainisha klichotokea, hatua za kiusalama zilizochukuliwa na kubaini ni nani hasa aliyehusika na ukatili huo.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.