MISRI-AJALI-USALAMA
Misri: Saba waangamia katika ajali ya helikopta Sinai
Helikopta iliyokuwa ikisafirisha askari wa Kikosi cha Waangalizi wa Kimataifa (MFO) huko Sinai nchini Misri imeanguka Alhamisi, na kuua askari saba, chanzo kutoka Israeli kimebaini.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wamarekani watano, Mfaransa mmoja na askari mmoja wa Jamhuri ya Czech, ni miongoni mwa askari waliopoteza maisha, chanzo hicho kimeongeza.
Ofisi ya MFO nchini Israeli imethibitisha ajali hiyo ya helikopta lakini imekataa kutoa maoni yake kwa kusubiri uchunguzi.
Mpaka sasa hazijafahamika sababu za ajali hiyo, na tayari uchunguzi umeanzishwa kulingana na chanzo hicho kutoka Israel.