Pata taarifa kuu
DRC-SIASA-USALAMA

Mvutano waendelea kujitokeza DRC kuelekea Uchaguzi mkuu

Wanaharakati wanaomuunga mkono rais Joseph Kabila nchini DRC wanaojiita FCC, wamezindua mkakati wa kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu mwezi Desemba mwaka huu.

Rais Joseph Kabila hajatangaza ikiwa atawania katika Uchaguzi mkuu ujao au la.
Rais Joseph Kabila hajatangaza ikiwa atawania katika Uchaguzi mkuu ujao au la. REUTERS/Kenny Katombe
Matangazo ya kibiashara

Hata hivyo, hawajaeleza iwapo rais Kabila atawania muhula wa tatu kinyume cha Katubaya nchi hiyo, licha ya kuonekana kumtaka kufanya hivyo, baada ya kumtaja kuwa ndio kiongozi wao.

Wakati wa hotuba yake wakati wa kuadhimisha miaka 58 ya Uhuru mwishoni mwa juma lililopita, rais Joseph Kabila aliswahakikishia wananchi wa DRC kuwa Uchaguzi Mkuu wa mwezi Desemba utafanyika kama ilivyopangwa lakini, Maaskofu wa Kanisa Katoliki wanasema wana mashaka iwapo Uchaguzi huo utafanyika.

Uchaguzi nchini DRC umepangwa kufanyika mnamo mwezi Desemba, na mivutano ya kisiasa bado inaendelea kuhusu uchaguzi huo. Baadhi ya wanasiasa wa upinzani wanataka uchaguzi huo ufanyike bila Kabial kuepo. Na wengine wanataka rais Joseph Kabila ashiriki katika uchaguzi huo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.