Kimbunga chaua watu 15 Somaliland, katika Pembe ya Afrika
Watu wasiopungua15 wamepoteza maisha Somaliland kutokana na mvua zenye upepo mkali kufuatia kimbunga Sagar, ambacho kilipiga Pembe ya Afrika mwishoni mwa wiki hi iliyopita, mamlaka imesema.
Imechapishwa:
omaliland, eneo la kaskazini mwa Afrika Mashariki na kwenye Ghuba ya Aden, lilijitenga kutoka Somalia mwaka 1991.
Katika Puntland, eneo linalojitawala kaskazini-mashariki mwa Somalia, mafuriko yaliyosababishwa na dhoruba iliyochanganyika na mvua viliuawa watu na mali zao hasa magari kwenye bonde la Bosaso, Yusuf Mohamed Waeys, gavana wa mko wa Bari, Puntland, aliliambia shiorika la habari la Reuters siku ya Jumapili.
Mvua zinazoendelea kunyesha Afrika Mashariki zimesababisha maafa makubwa hasara kubwa kwa mali na mashamba.