Afisa wa shirika la kihisani atekwa nyara Niger
Afisa wa shirika la kutoa misaada kutoka Ujerumani anaendelea kushikiliwa na kundi la watu wenye silaha ambao hawajulikani walipo, baada ya kukimbilia nchini Mali.
Imechapishwa:
Afisaa huyo alitekwa nyara siku ya Jumatano, Aprili 11, kaskazini mwa mji mkuu wa Niger, Niamey, katika jimbo la Ayorou. Alikua akifanya kazi kwa shirika lisilo la kiserikali la Help, linalohudumia wakimbizi kutoka Mali.
Afisa huyo alikuwa akitembea kwenye mtaa wa 18, katika eneo hatari, bila kusindikizwa na askari, wakati alitekwa.
Kundi la watu wenye silaha ambao walikua kwenye pikipiki ndio waliomteka nyara, baada ya kuzingira gari lake kilomita 25 kusini mwa mji wa Inatès, karibu na mpaka wa Mali.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo hilo, mfanyakazi huyo wa shirika la Help, ambaye alikua pamoja na raia wanne kutoka Niger, hakutoa upinzani wowote alipotekwa nyara.
Kabla ya kukimbilia kuelekea mpaka wa Mali, watekaji nyara hao walichoma moto gari la shirika hilo lisilo la kiserikali, na kuwashikilia kwa muda wa masaa kadhaa raia wanne wa Niger ikiwa ni pamoja na mwanamke, kabla ya kuwaachilia karibu na gari hilo lililokuwa likiteketea kwa moto.
Sio mara ya kwanza afisa huyu ambaye husaidia wakimbizi wa Mali kutembelea