Pata taarifa kuu
NIGERIA

Nigeria:Mashambulizi ya Boko Haram yasababisha vifo vya watu zaidi ya 30

Zaidi ya watu 30 wameuawa baada ya kutokea kwa milipuko mitatu ya kujitoa mhanga mjini Maiduguri Kaskazini mwa nchi ya Nigeria.

AFP PHOTO
Matangazo ya kibiashara

Ripoti zinasema kuwa mashambulizi hayo yalitekelezwa na wasichana watatu wanaoaminiwa kuwa kati ya miaka 11 na 15 mapema siku ya Ijumaa.

Shirika la kushughulikia majanga ya dharura linasema shughuli za kutafuta miili zaidi linaendelea pamoja na kuwapa hudumu za matibabu wale waliojeruhiwa.

Shambulizi hili la Ijumaa linakuja baada ya kutokea kwa shambulizi lingine kama hili siku ya Alhamisi lililosababisha vifo vya watu 32 katika mji huo wa Maiduguri.

Shambulizi la jana liliwalenga Waislamu waliokuwa wanaswali sala ya jioni na pia kusabibabisha majeraha.

Kundi la Boko Haram halijajitokeza kudai kutekeleza mashambulizi haya lakini maafisa wa usalama nchini humo wameendelea kulishuku.

Mwezi mmoja uliopita zaidi ya watu 100 wamepoteza maisha baada ya kutokea kwa mashambulizi kama haya ya kujitoa mhanga.

Kundi la Boko Haram limekuwa likitekeleza mashambulizi ya kigaidi kama haya tangu mwaka 2009 na serikali ya rais Muhamadu Buhari inasema inalenga kulitokomeza kudni hilo kufikia mwisho wa mwezi Novemba.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.