SIERRA LEONE-LIBERIA
Vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Ebola vyaongezeka Sierra Leone,Liberia
Idadi kubwa ya ripoti mpya za maambukizi ya virusi vya Ebola imetajwa huko Sierra Leone na Liberia ambapo kumearifiwa vifo 19 kutokea ndani ya siku tatu za juma hili,shirika la afya duniani WHO limearifu.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Idadi hiyo inaonesha kwamba ni harakati dhidi ya muda wa kudhibiti ugonjwa huo huko Sierra Leone, wameeleza madaktari wasio na mipaka.
Kwa ujumla kumetokea vifo 539 huko Afrika Magharibi tangu kutokea kwa ugonjwa huo katika taifa jirani la gine mnamo mwezi wa pili.
Viongozi katika ukanda huo wamekubaliana kuchangisha fedha kwa ajili ya kukabiliana na kuenea kwa ugonjwa huo.