Joyce Banda aongoza maelfu ya wananchi wa Malawi kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Bingu wa Mutharika
Rais wa Malawi Joyce Banda hii leo amewaongoza maelfu ya wananchi kwenye ukumbi wa bunge la nchi hiyo kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Bingu wa Mutharika.
Imechapishwa:
Zaidi ya wananchi elfu tatu wameripotiwa kuhudhuria tukio hilo ambapo wengi wao walikuwa wakitokwa na machozi mara baada ya kuuona mwili wa kiongozi wao.
Mutharika alifariki dunia majuma kadhaa yaliyopita akiwa nchini Afrika kusini ambako alikwenda kupatiwa matibabu ya maradhi ya moyo ambayo yamekuwa yakimsumbua kwa muda mrefu kiongozi huyo.
Mwili wa Mutharika aliwasili nchini humo siku ya jumamosi ukitokea Afrika kusini ambapo shughuli za mazishi zinaendelea kwa wananchi kupata fursa ya kuuga mwili wa marehemu kabla ya kuzikwa.
Kiongozi huyo anatarajiwa kuzikwa jumatatu ijayo kijijini kwake nje kidogo ya mji wa Blantyre.
Marehemu Mutharika atakumbukwa kwa juhudi zake za kutokomeza umasikini nchini humo pamoja na kupambana na rushwa.