Pata taarifa kuu
Côte d’Ivoire

Mamadou Koulibaly kiongozi wa muda wa chama cha FPI ajiuzulu na kupania kujiunga na chama kipya

Kiongozi wa muda wa chama cha aliyekuwa rais wa Côte d’Ivoire Laurent Gbagbo, Mamadou Koulibaly, ametangaza kujiuzulu kutoka uongozi wa chama chake kwa kuwa viongozi wa chama hicho wamekataa hatua ya kufanya mabadiliko katika chama hicho.

Mamadou Koulibaly,Spika wa bunge la Côte d’Ivoire
Mamadou Koulibaly,Spika wa bunge la Côte d’Ivoire AFP/Kambou Sia
Matangazo ya kibiashara

Koulibaly, spika wa bunge la cote d ivoire, aliyekuwa kiongozi wa muda wa chama cha Ivorian People's Front(FPI) baada ya kuanguka kwa gbagbo, amesema anajiuzulu na hivi sasa anataka kujiunga na chama kipya kitakachoitwa Freedom and Democracy for the republic ,wakati huu wakielekea kwenye uchaguzi wa ubunge.

Koulibaly amesema Uongozi wa FPI unaona kuwa kubadilisha mtazamo wa chama ni kuwasaliti wafuasi wa chama hicho waliofungwa na walio uhamishoni.

Koulibaly ameleta mkanganyiko ndani ya chama kwa kukosoa vikali namna ambavyo Ggbagbo alikuwa akijihusisha na machafuko ya kisiasa na mwenendo mzima wa chama kipindi alichokuwa madarakani.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.