Bunge la Gabon laondoa kinga kwa kiongozi aliyejitangaza Rais na kuunda serikali
Wabunge nchini Gabon jana walipiga kura kuondoa kinga kwa kiongozi wa upinzani Andre Mba Obame ambaye alijitangaza mshindi wa uchaguzi wa Urais,na hatua hiyo imefungua njia ya kufunguliwa mashtaka kwa kiongozi huyo wa upinzani.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Hatua hiyo imekuja baaada ya waziri wa sheria wa Gabon Ida Assonouet kuwasilisha ombi la kuondolewa kwa kinga hiyo katika barua aliyomwandikia spika wa bunge la nchi hiyo March Kumi na nne mwaka huu.
Mba obame waziri wa zamani wa mambo ya ndani wa Gabon alijitangaza mshindi wa urais wa mwaka 2009 uliomweka madarakani rais Ali Bongo ,hatua iliyoelezewa na waziri wa sheria kuwa ilihatarisha mno usalama wa nchi hiyo.
Chama chake kilivunjwa tarehe 27 january mwaka huu.