Rais wa Benki ya Dunia ajiuzulu
Rais wa Benki ya Dunia, Jim Yong Kim ametangaza kuwa, atajizulu wadhifa huo mwezi ujao, miaka mitatu kabla ya muda wake kumalizika.
Imechapishwa:
Hatua hii inatarajiwa kumpa Rais wa Marekani Donald Trump, fursa ya kushawishi kiongozi mpya wa Benki inayolenga kumaliza umasikini duniani.
Chini ya uongozi wake, Kim alikuwa amejiwekea malengo ya Benki hiyo kumaliza umasikini kufikia mwaka 2030.
Katika taarifa yake, Jim Yong Kim, ambaye amekuwa akiongoza Benki ya Dunia kwa miaka sita, amesema tu kwamba atajiunga na "kampuni ya uwekezaji" na kuzingatia "uwekezaji wa miundombinu katika nchi zinazoendelea."
I will be stepping down as @worldbank Group president on February 1. It’s been the greatest privilege I could have ever imagined to lead the dedicated staff of this great institution to bring us closer to a world that is finally free of poverty. https://t.co/jWGoihu7tu
Jim Yong Kim (@JimYongKim) January 7, 2019