ISRAEL-UCHUMI-UFISADI
Netanyahu aishtumu polisi kufuatia madai ya ufisadi
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kupitia ukursa wake wa Facebook amewashtumu wapelelezi katika jeshi la polisi wanaomchunguza kwa madai ya ufisadi.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Netanyahu amesema inashangaza kwa Kamishena wa Polisi anawatumia wachunguzi binafsi yake.
Mapendekezo ya wachunguzi hao wanatarajiwa kuwasilishwa kwa mwanasheria mkuu wa serikali wiki ijayo.
Ripoti zinasema kuwa miongoni mwa mapendekezo hayo ni kutaka Netanyahu kuchunguzwa rasmi kwa madai ya ufisadi, na ubadhirifu.
Serikali imekataa kuzungumzia madai haya.