Pata taarifa kuu
BRAZIL-RUSHWA-HAKI

Aliyekua rais wa Brazil apigwa marufuku kuwania urais

Rais wa zamani wa Brazil Luiz Inacio "Lula" da Silva amepigwa marufuu kuwania urais wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka huu, baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya ufisadi.

Aliye kuwa rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva, anashtumiwa kupewa hongo na shirika la mafuta la serikali la Petrobas.
Aliye kuwa rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva, anashtumiwa kupewa hongo na shirika la mafuta la serikali la Petrobas. REUTERS/Paulo Whitaker
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii imekuja baada ya Mahakama ya Rufaa kushikilia hukumu ya ufisadi dhidi yake na kuongeza kifungo chake jela kutoka miaka miaka tisa hadi miaka 12 na mwezi mmoja.

Rais huyo wa zamani ameendelea kukanusha kuwa alijihusisha na ufisadi na kuongeza kuwa, ameendelea kulengwa kisiasa.

Wafuasi wake wamasema Uchaguzi wa mwezi Oktoba bila Lula, sio uchaguzi. Wachambuzi wa siasa wanasema iwapo angewania anaweza kushinda.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.