Marekani yatishia kusitisha misaada yake kwa Pakistan
Rais wa Marekani Donald Trump amesema Marekani itasitisha misaada yake kwa nchi ya Pakistan kwa sababu imeendelea kuidanganya Marekani kwa muda mrefu.
Imechapishwa:
Rais Trump ameandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa Pakistan inawapa hifadhi magaidi, ambao wanatafutwa na wanajeshi wa Marekani walioko nchini Afghanistan, na kwamba kwa muda mrefu imekuwa ikiwaficha.
The United States has foolishly given Pakistan more than 33 billion dollars in aid over the last 15 years, and they have given us nothing but lies & deceit, thinking of our leaders as fools. They give safe haven to the terrorists we hunt in Afghanistan, with little help. No more!
Donald J. Trump (@realDonaldTrump) 1 janvier 2018
Rais wa Marekani pia ameongeza kuwa Pakistan imepokea msaada wa jumla ya dola bilioni Thelathini na nne katika kipindi cha miaka 15 iliyopita na kwamba licha ya makubaliano waliyoafikia hakuna chochote kilichotekelezwa ila uongo na ulaghai, wakifikiria kuwa viongozi wa Marekani hawana akili timamu, amesema Trump.
Marekani inadhamiria kuendelea kuzuia zaidi ya milioni 250 ya msaada kwa Pakistan, ambayo ilichelewesha kwa makusudi kupelekwa kwa taifa hilo la barani Asia, tangu mwezi Agosti mwaka jana.
Wakati huo, Wizara ya mambo ya nje ya Pakistan, iliahidi kuwa itazidisha juhudi zake za kimataifa za kupambana na magaidi.