Gurudumu la Uchumi
Changamoto na mafanikio ya kiuchumi ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania
Imechapishwa:
Cheza - 10:16
Mtangazaji wa makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili ameangazia miaka 53 ya muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania, licha ya muungano huu kudumu kumekuwa na changamoto za kiuchumi na kisiasa ambazo zimeendelea kushuhudiwa na kuleta sintofahamu kuhusu mgawanyo wa rasilimali na mgawanyo wa fedha za muungano.Mtangazaji wa makala haya amezungumza na mtaalamu wa masuala ya uchumi pamoja na yule wa kisiasa kuangazia changamoto na mafanikio ya muungano huu kiuchumi na kwa bara la Afrika.