Uchaguzi wa Donald Trump, pigo kwa raia wengi wa Cuba
Ushindi wa Donald Trump katika uchaguzi wa urais nchini Marekani umepokelewa na wasiwasi na Wacuba wengi. Kwa uhakika, wanahofia kuona juhudi za kufufua uhusiano kati ya nchi yao na Marekani zinaweza kuambulia patupu.
Imechapishwa:
Mfanyabiashara huyo tajiri wa Marekani aliwahi kusikika akisema kuwa atarejelea baadhi ya mambo yaliyoafikiwa na Barack Obama kwa utawala wa kikomunisti katika maamuzi ya kuzuia mali za Cuba mwishoni mwa mwaka 2014.
Kufuatia hali hiyo, Rais wa Cuba Raul Castro, mtetezi pamoja na mwenzake wa Marekani Barack Obama, wa kufufua uhusianokati ya Washington na Havana, amempongeza Donald Trump, mshindi wa uchaguzi wa urais wa Marekani Jumatano, Novemba 9.
Serikali ya Cuba imetangaza katika gazeti la serikali kufanyika katika siku za usoni kwa mazoezi mapya muhimu ya kijeshi kwa lengo la kukabiliana na uwezekano wa uvamizi.
Kama harakati hizi zitawekwa katika vitendo, huenda hali ikawa mbaya zaidi katika siku za usoni kuhusu uhusiano kati ya maadui wawili wa zamani wa vita baridi wakati Trump atachukua hatamu ya uongozi wa nchi mwezi Januari mwakani.
Nchini Cuba, wakazi wengi tayari wameonyesha wasiwasi wao juu ya uchaguzi wa Donald Trump. Bw, Trump alitangaza miezi ya hivi karibuni keamba anapinga uamuzi wa kufutwa vikwazo vya kifedha na kibiashara vilivyowekewa Cuba tangu 1962.
Wapinzani wa Castro wamuunga mkono Donald Trump
Uchaguzi wa Donald Trump umesababisha raia wengi wa Cuba kukata tamaa. Donald Trump alipozuru Florida tarehe 21 Oktoba, wakati alikuwa bado mgombea, alikutana na wapinzani wa utawala wa kikomunisti na alisema anawaunga mkono kwa harakati zao.