Pata taarifa kuu
TANZANIA-TWITTER-DAR ES SALAAM

Michezo mbalimbali kufanyika katika tamasha la watanzania wanaotumia mtandao wa Twitter

Watanzania watumiaji wa mtandao wa Twitter wanakutana kesho katika tamasha litakalohusisha mambo mbalimbali ikiwemo michezo.

Watu waliohudhuria katika tamasha la pili lililowakutanisha watanzania wanaotumia mtandao wa Twitter
Watu waliohudhuria katika tamasha la pili lililowakutanisha watanzania wanaotumia mtandao wa Twitter Twitter
Matangazo ya kibiashara

Tamasha hilo litafanyika katika Viwanja vya posta vilivyopo Kijitonyama Mjini Dar es Salaam.

Hili litakuwa tamasha la tatu tangu kuasisiwa kwake mwaka mmoja uliopita likiratibiwa na mmoja wa waasisi wake Fred Kavishe.

Mkurugenzi wa Benki ya dunia Tanzania, Malawi na Burundi Bella Bird akiwa na mmoja wa waasisi wa tamasha la TOT Bonanza Fred Kavishe
Mkurugenzi wa Benki ya dunia Tanzania, Malawi na Burundi Bella Bird akiwa na mmoja wa waasisi wa tamasha la TOT Bonanza Fred Kavishe The Citizen

Mbali na michezo kama riadha, soka pia kutakuwa na huduma mbalimbali ikiwemo za elimu ya haki  za binadamu itakayotolewa na kituo cha sheria na haki za binadamu Tanzania, LHRC na taasisi nyingine zikiwemo za kibenki.

Tayari kumekuwa na tambo mbalimbali kupitia mtandao wa Twitter ambapo watumiaji wamekuwa wakielezea hisia zao kuelekea tamasha hilo.

Waziri wa Viwanda wa Tanzania Innocent Bashungwa ametumia ukurasa wake wa Twitter kuonyesha nia ya kuhudhuria tamasha hilo

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.