Pata taarifa kuu
UFARANSA-HUGO LLORIS-TOTTENHAM HOTSPURS

Kipa wa Ufaransa kukosa msimu uliosalia wa ligi kuu ya Uingereza 2019/20

Kipa wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Tottenham Hotspurs ya Uingereza Hugo Lloris atakosa msimu wote wa ligi kuu ya Uingereza baada ya kuumia kiwiko mwishoni mwa wiki iliyopita. 

Golikipa wa Tottenham Hotspurs Hugo lloris akitolewa nje ya uwanja baada ya kupata jeraha la mkono katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Brighton
Golikipa wa Tottenham Hotspurs Hugo lloris akitolewa nje ya uwanja baada ya kupata jeraha la mkono katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Brighton BBC
Matangazo ya kibiashara

Lloris alipata jeraha hilo wakati wa mchezo wa ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Brighton ambao ulimalizika kwa Spurs kubandikwa mabao 3-0.

Golikipa huyo wa Ufaransa alishindwa kuokoa kikamilifu mpira wa mchezaji wa Brighton Pascal Gross katika kipindi cha kwanza cha mchezo.

Taarifa ya klabu hiyo hata hivyo inasema mchezaji huyo hatahitaji kufanyiwa upasuaji na kueleza kwamba mchezaji huyo ataonekana tena uwanjani msimu ujao.

Lloris amekuwa kwenye kiwango cha juu tangu alipojiunga na klabu hiyo na mwaka 2018 alikuwa kipa wa kwanza kwenye kikosi cha Ufaransa kilichoshinda kombe la dunia katika fainali zilizofanyika nchini Urusi.

Hugo Lloris akiwa na kikosi cha ufaransa kilichoshinda fainali za kombe la dunia mwaka 2018
Hugo Lloris akiwa na kikosi cha ufaransa kilichoshinda fainali za kombe la dunia mwaka 2018 wikipedia

Spurs inasema mchezaji huyo anahitaji kupumzika na kufanuya mazoezi ya taratibu.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.