Pata taarifa kuu
TANZANIA-KENYA-BURUNDI-AFCON 2019-SOKA

Nchi tatu za Afrika mashariki zaanza vibaya AFCON

Timu za taifa za mchezo wa soka za Kenya na Tanzania, zimeanza vibaya michuano inayoendelea kuwania taji la bara Afrika nchini Misri, huku baadhi ya mataifa yakiendelea vizuri.

Kikosi cha timu ya taifa ya Burundi Intamba mu Rugamba.
Kikosi cha timu ya taifa ya Burundi Intamba mu Rugamba. RFI-KISWAHILI
Matangazo ya kibiashara

Taifa Stars ilikuwa timu ya kwanza kufungwa na Senegal mabao 2-0 na baadaye Harambee Stars kupoteza pia kwa mabao 2-0 dhidi ya Algeria, katika mechi za kundi C.

Wawakilishi hao wa Afrika Mashariki, walionekana kuelemewa katika mechi zao, na watanarajiwa kumenyana baadaye wiki hii.

Burundi na DRC ni timu nyingine zinazowakilisha ukanda wa Afrika, zilizoanza vibaya, lakini Uganda ilianza kwa matumaini baada ya kuishinda DRC mabao 2-0.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.