TANZANIA-KENYA-BURUNDI-AFCON 2019-SOKA
Nchi tatu za Afrika mashariki zaanza vibaya AFCON
Timu za taifa za mchezo wa soka za Kenya na Tanzania, zimeanza vibaya michuano inayoendelea kuwania taji la bara Afrika nchini Misri, huku baadhi ya mataifa yakiendelea vizuri.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Taifa Stars ilikuwa timu ya kwanza kufungwa na Senegal mabao 2-0 na baadaye Harambee Stars kupoteza pia kwa mabao 2-0 dhidi ya Algeria, katika mechi za kundi C.
Wawakilishi hao wa Afrika Mashariki, walionekana kuelemewa katika mechi zao, na watanarajiwa kumenyana baadaye wiki hii.
Burundi na DRC ni timu nyingine zinazowakilisha ukanda wa Afrika, zilizoanza vibaya, lakini Uganda ilianza kwa matumaini baada ya kuishinda DRC mabao 2-0.