Real Madrid ndio klabu yenye thamani kubwa zaidi Ulaya
Klabu ya Real Madrid ya nchini Hispania imeipiku Manchester United ya Uingereza kama timu yenye thamani kubwa zaidi barani Ulaya, ambapo ina utajiri wa paundi bilioni 3.22, imesema ripoti ya kampuni ya mahesabu na ukaguzi KPMG.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Ripoti hii ambayo imejikita katika mauzo ya biashara kwa mwaka wa fedha 2016-17 na 2017-18, ilitazama faida iliyotokana na matangazo mubashara, umaarufu, vifaa vya michezo na thamani ya uwanja.
Klabu za Tottenham na Liverpool ambazo zitacheza mchezo wa fainali ya klabu bingwa barani Ulaya, zenyewe zinashika nafasi ya 7 na 9 kwenye orodha hiyo.
Klabu za Chelsea na Arsenal ambazo zitacheza mchezo wa fainali ya kombe la Europa League, zenyewe zinashika nafasi ya 6 na 8.
Manchester City yenyewe iko kwenye nafasi ya 5, hii ikimaanisha kuwa kuna jumla ya timu 6 za kutoka ligi kuu ya Uingereza katika jumla ya timu 10 zenye thamani.
Real Madrid ilishinda taji la klabu bingwa Ulaya kwa misimu miwili mfululizo ambapo takwimu hizi zilijumuisha, ikiongeza thamani yake kwa asilimia 10.
Klabu ya Scotland ya Celtic imo kwenye orodha ya timu 32 ikiwa ni timu ya kwanza kufanya hivyo.
Mkurugenzi wa KPMG, Andrea Sartori amesema kiujumla thamani ya vilabu vya Ulaya imeongezeka kwa asilimia 9 katika mwaka uliopita.
KPMG inasema kwa upande mwingine gharama za wafanyakazi zimeongezeka, ambapo gharama zao zimeongezeka kwa asilimia 4 na kufikia asilimia 63.
IFUATAYO NI ORODHA YA TIMU 10 ZENYE THAMANI ULAYA
Real Madrid - €3.224bn
Manchester United - €3.207bn
Bayern Munich - €2.696bn
Barcelona - €2.676bn
Manchester City - €2.460bn
Chelsea - €2.227bn
Liverpool - €2.095bn
Arsenal - €2.008bn
Tottenham - €1.697bn
Juventus - €1.548bn