Mechi kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika kupigwa katika viwanja mbalimbali
Michuano ya hatua ya makundi, kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika inaendelea leo Ijuma na kesho Jumamosi katika mataifa mbalimbali barani Afrika.
Imechapishwa:
Orlando Pirates ya Afrika Kusini itacheza na FC Platinum ya Zimbabwe katika mechi ya kundi B, huku Esperance de Tunis ya Tunisia ikimenyana na Horoya ya Guinea.
Kundi C, Ismail ya Misri itamenyana na TP Mazembe ya DRC, huku CS Constantune ya Algeria ikiwa nyumbani kucheza na Club Africain ya Tunisia.
Kesho mechi za kundi D:
AS Vita Club itacheza na Al-Ahly, huku JS Soura ikichuana na Simba FC ya Tanzania.
Kundi A :
ASEC Mimosa ya Cote Dvoire itakuwa nyumbani kucheza na Wydad Casablanca huku Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ikichuana na Lobi Stars.