Baada ya kushinda Tanzania kwa bao la ugenini, Burundi itamenyana na Congo Brazaville, licha ya kushinda mabao 3-1, vijana wa Tanzania waliondolewa kwa sababu Burundi walikuwa wamepata ushindi nyumbani wa mabao 2-0 na kuruhusu bao katika mechi ya Jumanne kuliwaharubia mambo.
Kenya itacheza na Sudan, baada ya kufanikiwa kuishinda Mauritius kwa jumla ya mabao 8-1, huku Sudan ikiilemea Ushelisheli kwa jumla ya mabao 2-1.
DRC nayo itamenyana na Morocco, baada ya kuilemea Rwanda kwa jumla ya mabao 5-0.
Ethiopia nayo itamenyana na Mali. Mechi hizi, zitachezwa nyumbani na ugenini na mshindi atafuzu latika mzunguko wa tatu na wa mwisho, ili kutafuta timu nane bora kutafuta ubingwa wa Afrika.