Pata taarifa kuu
KENYA-CAF-SOKA

Emerging Stars wajiweka kwenye nafasi nzuri

Timu ya taifa ya soka ya Kenya, inayowajumuisha wachezaji wenye chini ya umri wa miaka 23, walianza vema kampeni ya kufuzu katika fainali ya bara Afrika mwaka 2019 nchini Misri, baada ya kuifunga Mauritus mabao 5-0.

Beki wa timu ya taifa ya soka ya Kenya, inayowajumuisha wachezaji wenye chini ya umri wa miaka 23, Johnstone Omurwa (katikati) kisherehekea bao la kwanza dhidi ya Mauritiusakiwa pamoja na Joseph Okumu na Chrispinus Onyango.
Beki wa timu ya taifa ya soka ya Kenya, inayowajumuisha wachezaji wenye chini ya umri wa miaka 23, Johnstone Omurwa (katikati) kisherehekea bao la kwanza dhidi ya Mauritiusakiwa pamoja na Joseph Okumu na Chrispinus Onyango. Football Kenya Federation/twitter.com
Matangazo ya kibiashara

Emerging Stars, ilipata ushindi huo mkubwa katika mechi iliyochezwa siku ya Jumatano jioni latika uwanja wa Kimataifa wa Kasarani jijini Nairobi.

Mabao ya Johnston Omurwa, James Mazembe, Piston Mutamba, Sidney Lokale na Joseph Okumu yanaiweka Kenya katika nafais nzuri ya kufuzu katika hatua ya pili ya michuano hiyo, itakaporudiana na Mauritius tarehe 18 mwezi huu.

Matokeo zaidi:-

Burundi2-0 Tanzania

Ethiopia 4-0 Somalia

Rwanda 0-0 DRC

Uganda 1-0 Sudan Kusini

Ushelisheli 1-1 Sudan

Mataifa nane yatafuzu kushiriki katika fainali hiyo. Nigeria ndio mabingwa watetezi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.