Mechi za Ligi ya Europa kuchezwa leo barani Ulaya
Michuano ya Europa League kwa ngazi ya klabu inaendelea leo kwa mechi mbalimbali kuchezwa katika Miji tofauti barani Ulaya.
Imechapishwa:
Mashindano hayo ni ya pili kwa ukubwa kwa ngazi ya klabu barani Ulaya, yakitanguliwa na michuano ya Ligi ya mabingwa Ulaya.
RB Leipzg itakuwa mgeni wa Celtic ya Scotland, Arsenal imesafiri hadi nchini Ureno ambako itachuana na Sporting Lisbon wakati Chelsea ya Uingereza itaipokea BATE Borisov ya Bulgaria.
Mechi nyingine ni kama ifuatavyo.
Rangers itachuana na Spartak Moscow
RB Salzburg itachuana na Rosenburg ya Norway
Zenit St Petersburg itachuana na Bordeaux ya Ufaransa
Anderlect ya Ubelgiji itapambana na Fenerbance ya Uturuki
FC Copenhagen itapambana na Slavia Prague