Pata taarifa kuu
UN-KENYA-RIADHA-KIPCHOGE

Eliud Kipchoge atuzwa na Umoja wa Mataifa

Bingwa wa dunia wa mbio za Marathon nchini Kenya Eliud Kipchoge ametajwa kuwa mtu wa mwaka wa Umoja wa Mataifa kwa mwaka 2018.

Bingwa wa dunia wa mbio za Marathon Eliud Kipchoge baada ya kutuzwa na Umoja wa Mataifa jijini Nairobi Oktoba 24 2018
Bingwa wa dunia wa mbio za Marathon Eliud Kipchoge baada ya kutuzwa na Umoja wa Mataifa jijini Nairobi Oktoba 24 2018 twitter.com
Matangazo ya kibiashara

Mwanariadha huyo wa miaka 33, amepata tuzo hiyo katika Ofisi za Umoja huo jijini Nairobi, baada ya kuvunja rekodi ya mashindano ya Berin Marathon mwezi Septemba kwa muda wa saa mbili dakika moja na sekunde 39.

Aidha, Umoja wa Mataifa umempongeza kwa jitihada zake za kutoa elimu kuhusu namna ya kupambana na maambukizi ya ugonjwa hatari wa Ukimwi.

Kipchoge, anaelezwa kuwa Mwanariadha bora duniani katika mbio za Marathon baada ya kukimbia kwa kasi na kushinda mashindano ya Berlin na London Marathon mara tatu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.