Equity Bank Hawks yashinda ubingwa kanda ya tano mchezo wa kikapu
Klabu ya wanawake ya Equity Bank Hawks kutoka nchini Kenya ndio mabingwa wa kanda ya tano ya mashindano ya Afrika katika mchezo wa Kikapu yaliyomalizika jijini Dar es salaam nchini Tanzania mwishoni mwa juma lililopita.
Imechapishwa:
Fainali ilizikutanisha klabu zote kutoka nchini Kenya, mabingwa hao wapya na klabu ya Bandari KPA.
Mabingwa hao walionekana imara katika idara zote na kupata ushindi wa vikapu 24-17, 19-9 na 201-15 katika mizunguko mitatu ya mchezo huo.
Hata hivyo, KPA, walipata ushindi wa mzunguko wa mwisho wa vikapu 13-7, lakini Equity Bank Hawks wakapata ushindi wa jumla kwa kupata vikapu 70-54.
Kocha David Maina amefurahishwa na ushindi huo na kusema, wachezaji wake walikuwa wazuri katika mechi hiyo.
“Tulikuwa bora kuwazidi KPA katika mchuano huu, na tulikuwa imara sana, ni mafanikio makubwa kwa klabu hii iliyoanza miaka mitano iliyopita,” alisema kocha Maina.
Nayo klabu ya wanaume ya KPA, ilipoteza nafasi ya tatu, baada ya kufungwa na Energy Group ya Rwanda kwa vikapu 74-71.