CHELSEA-SOKA-UINGEREZA
Chelsea yamtangaza Sarri kuwa meneja wake mpya
Klabu ya Chelsea ya Uingereza imemtangaza muitaliano Maurizio Sarri kuwa meneja mpya kwa mkataba wa miaka mitatu.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Sarri aliyeiwezesha Napoli kumaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita amesaini mkataba wa miaka mitatu, anachukua nafasi ya Antonio Conte aliyefutwa kazi baada ya kuhudumu kwa misimu miwili.
Makocha wengine kutoka Italia waliowahi kuinoa Italia ni Roberto Di Matteo, Carlo Ancelloti na Claudio Ranieri.
Wakati huohuo, Chelsea imemsajili Jorginho, kiungo mbrazil wa Napoli kwa mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya Euro milioni 50