Pata taarifa kuu
FIFA-URUSI-KOMBE LA DUNIA 2018

Nusu fainali ya kwanza kombe la dunia, kuchezwa kesho

Nusu fainali ya kwanza ya kombe la dunia inachezwa kesho baina ya Ubelgiji na Ufaransa.

Wachezaji wa Ufaransa wakishangilia baada ya kuishinda Uruguay katika mchezo wa robo fainali
Wachezaji wa Ufaransa wakishangilia baada ya kuishinda Uruguay katika mchezo wa robo fainali REUTERS/Grigory Duko
Matangazo ya kibiashara

Mchezo huo ni muhimu kwa makocha wote, Roberto Martinez wa Ubelgiji na Didier Deschamps wa Ufaransa.

Deschamps anataka kuweka rekodi ya kushinda taji hili akiwa meneja baada ya kuiongoza Ufaransa kushinda taji hilo mwaka 1998 akiwa nahodha wa kikosi cha dhahabu.

Martinez kwa upande wake anaongoza kikosi cha dhahabau kinachotajwa kuwa na wachezaji wengi nyota katika historia ya soka la Ubelgiji.

Ebelgiji iliwaondoa Brazil katika hatua ya robo faainali kwa mabao 2-1 wakati Ufaransa iliinyuka Uruguay kwa mabao 2-0.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.