FIFA-URUSI-KOMBE LA DUNIA 2018
Nusu fainali ya kwanza kombe la dunia, kuchezwa kesho
Nusu fainali ya kwanza ya kombe la dunia inachezwa kesho baina ya Ubelgiji na Ufaransa.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mchezo huo ni muhimu kwa makocha wote, Roberto Martinez wa Ubelgiji na Didier Deschamps wa Ufaransa.
Deschamps anataka kuweka rekodi ya kushinda taji hili akiwa meneja baada ya kuiongoza Ufaransa kushinda taji hilo mwaka 1998 akiwa nahodha wa kikosi cha dhahabu.
Martinez kwa upande wake anaongoza kikosi cha dhahabau kinachotajwa kuwa na wachezaji wengi nyota katika historia ya soka la Ubelgiji.
Ebelgiji iliwaondoa Brazil katika hatua ya robo faainali kwa mabao 2-1 wakati Ufaransa iliinyuka Uruguay kwa mabao 2-0.