KOMBE LA DUNIA-UFARANSA-UBELIGIJI-URUSI
Ufaransa, Ubelgiji ni kufa au kupona Kombe la dunia
Timu za Taifa za Ufaransa 'Le Blues' na Ubelgiji zinaendelea na maandalizi kabambe kabla ya kuchuana jumanne, ukiwa ni mchezo wa kwanza wa hatua ya nusu fainali ya Kombe la dunia.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Ufaransa ilifika hatua hiyo baada ya kuishinda Uruguay kwa mabao 2-0 wakati Ubelgiji iliiangusha Brazil kwa mabao 2-1.
Ufaransa itategemea zaidi wachezaji Antoine Griezman na Kylian Mbappe wakati Ubelgiji inayoundwa na nyota mbalimbali itategemea kiungo wa chelsea Eden Hazard na Romelu Lukaku.
Mshindi baina ya Ufaransa na Ubelgiji atachuana na mshindi baina ya England na Croatia katika fainali itakayochezwa Julai 15.